EXCLUSIVE PICTURE...
Kocha wa zamani wa Simba, Milovan
Cirkovic ameondoka katika ardhi ya Tanzania baada ya kukwea pipa leo saa 10:30
alfajiri.
Milovan aliyewasili kwenye Uwanja
wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA), alizungumza na mtandao huu na
kueleza mambo mengi kuhusiana na Simba.
Kila kitu alichoeleza Milovan
kuhusiana na maisha yake wakati akiwa Simba kitawekwa hewani.
Kocha huyo ambaye amelipwa fedha
zake dola 32,000 na nyongeza ya dola 3,000 kutoka kwa Malkia wa nyuki ameanika
mambo mengi sana.
Lakini amerudia tena kuwashukuru
mashabiki wa Simba kwa kuonyesha ushirikiano mkubwa na anawatambua kama ndugu.
Kocha huyo ameondoka na rekodi ya
ubingwa Simba ikiwa ni pamoja na rekodi kubwa ya ushindi ‘mnene’ wa mabao 5-0
dhidi ya watani wao Yanga, msimu uliopita.
Milovan aliondoka na dege la
Shirika la Ndege la Uturuki na anatajia kutua Belgrade, Serbia leo na
ataunganisha safari ya takribani saa mbili kwenda katika mji aliozaliwa wa
Cacak unaotamkwa chachak.
0 COMMENTS:
Post a Comment