Kocha Mkuu wa Yanga, Ernie Brandts ameamua kufanya kazi ya
kuwanoa wachezaji wanne ambao watakabidhiwa kupiga mipira ya faulo maarufu kama
‘iliyokufa’.
Brandts raia wa Uholanzi amesema tayari ameanza kazi hiyo
kwa kuwa anataka kikosi chake kiendelee kukamilika kila idara kila siku
zinavyosonga.
“Kawaida katika timu unaimarisha mambo hatua kwa hatua,
hivyo sasa tumefikia wakati wa kutengeneza wapiga faulo wa uhakika.
“Nitateua wachezaji wanne ambao nitakuwa nikifanya nao kazi
hiyo kila ninapokuwa na nafasi ili kuhakikisha ikitokea faulo, tunaangalia iko
upande gani na anapiga nani,” alisema Brandts.
Kabla ya hapo, Athumani Idd ‘Chuji’ na Oscar Joshua ndiyo waliokuwa
wakipiga faulo nyingi za kikosi hicho.
0 COMMENTS:
Post a Comment