February 26, 2013




Pamoja na kulipwa fedha zake, kocha wa zamani wa Simba, Milovan Cirkovic amesema anaondoka nchini akiwa na majonzi makubwa.

Milovan raia wa Serbia amesema kulipwa fedha zake kwa maana ya maslahi lilikuwa ni jambo muhimu sana, lakini urafiki wake na watu wa Simba ni muhimu zaidi moyoni mwake.

“Naona naondoka nawaacha rafiki zangu wa kweli, angalia mashabiki walivyoniunga mkono kuanzia mwanzo hadi. Tokea nikiwa na timu hadi wakati wa matatizo.

“Mashabiki wa Simba walikuwa na ujasiri mkubwa, ingawa kuna baadhi ya viongozi walionyesha chuki ya wazi dhidi ya yangu, lakini bado wao waliendelea kuonyesha upendo.

“Nasikia faraja kwa kuwa zaidi ya watu milioni waliniunga mkono na wawili au watatu tu wakaonyesha chuki kwangu, haliwezi kuwa suala gumu kwangu. Nitaendelea na mambo yangu na sitaacha kuikumbuka Simba kwa kuwa wengi wao wananipenda.

“Naipenda sana Simba, wakati mwingine natamani ingekuwa kwetu Serbia. Lakini maisha ndivyo yalivyo, siku ya mwisho mambo hubadilika na unatakiwa kukubali.

"Wako ambao sasa wananishambulia, najua hawakupenda nipate haki yangu, lakini inawauma ninavyosema ukweli. Siku wakitulia watakubali ninachokisema kwa kuwa wanakijua na wanaelewa kilivyotokea, mimi si mgomvi, pia sipendi malumbano” alisema Milovan.

Mlezi wa Simba, Rahma Al Kharusi alijitolea kumlipa MIlovan fedha dola 32,000 alizokuwa anaudai uongozi wa Simba ambao ulikuwa ukimzungusha huku viongozi wake wakiendelea kutoa ahadi.

Rahma maarufu kama Malkia wa Nyuki alitoa kitita cha dola 35,000 ikiwa ni dola 3000 zaidi ya alichokuwa anadai kocha huyo na tayari ameishapokea fedha zake.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic