February 28, 2013




Aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Fat na baadaye TFF, Michael Wambura amesema iwapo Tanzania itafungiwa na Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa), anayepaswa kulaumiwa ni Rais wa shirikisho hilo, Leodeger Chilla Tenga.

Wambura amesema matatizo yaliyojitokeza wakati wa upitishwaji wa katiba mpya ya TFF iliyokataliwa na serikali yalitokana na usimamizi mbovu wa shirikisho hilo.

Akizungumza leo na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Wambura alisema Tenga ndiye atakuwa wa kulaumiwa kama kiongozi wa juu kabisa wa shirikisho ambalo lilifanya mabadiliko hayo ya katiba kiholela.

Aidha, Wambura alimtaka Tenga kuwaomba radhi Watanzania kutokana na matatizo yaliyojitokeza katika uchaguzi wa shirikisho hilo, hali iliyosababisha serikali kuamua kuingilia.

 “Tukienda kinyume na uamuzi wa serikali itakuwa ni utovu mkubwa wa nidhamu, nawasihi  wajipime kuhusiana na kujadili kuhusiana na uamuzi wa serikali kuifuta katiba mpya iliyokiuka sheria. Badala yake wafanye utekelezaji mara moja.

“Najua watafanya hivyo ikizingatiwa kati ya wajumbe wa kamati hiyo ni watumishi wa serikali,” alisema wambura.

Serikali iliingilia kati na kuifuta katiba mpya ya TFF iliyopitishwa kwa njia ya waraka, kitu ambacho kimeonekana ni ukiukwaji wa katiba ya TFF.

TFF ilisema iliamua kutumia waraka kupitisha marekebisho ya katiba kwa kuwa hawakuwa na fedha za kuitisha mkutano mkuu, kitu ambacho mwisho kimeonekana si sahihi.

Katiba hiyo mpya, tayari ilitumika kuwapiga panga baadhi ya wagombea akiwemo Jamal Malinzi aliyekuwa anawania nafasi ya Urais, akichuana na Athumani Nyamlani ambaye mwisho alibaki kuwa mgombea pekee.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic