March 1, 2013



BRANDTS AKIWA NA MMILIKI WA SALEHJEMBE, SALEH ALLY ALIPOMTEMBELEA OFISINI KWAKE JIJINI DAR ES SALAAM, JANA.

Kocha  Mkuu wa Yanga, Ernie Brandts amesisitiza bado timu yake inasumbuliwa na ugonjwa wa wachezaji wake hasa washambuliaji kutozitumia nafasi za kufunga wanazozipata.

Brandts raia wa Uholanzi amesema huo ndiyo ugonjwa mkubwa katika kikosi chake na amekuwa akiendelea kuufanyia kazi kwa juhudi kubwa.

Kocha huyo ambaye amekigeuza kikosi cha Yanga, ameiambia Salehjembe kuwa iwapo washambuliaji wake wangekuwa wakitumia vizuri nafasi wanazopata, kikosi chake kisingekuwa na hofu na mechi yoyote.

“Tuna kikosi kizuri na wachezaji wangu wanajitahidi sana, ingawa bado tunafanya mazoezi katika viwanja vyenye viwango vya chini lakini wanaonyesha tofauti kubwa katika mechi zetu.

“Tatizo kubwa ambalo naona ni kama ugonjwa ambao nautafutia tiba ni kupoteza nafasi, hali hiyo hainivutii, lakini bado naendelea kuifanyia kazi.

“Katika soka mambo mengine yanabadilika baada ya kuyazungumzia au kufanya mazoezi kwa siku kadhaa na si mara moja au mbili. Hata hivyo, nimekuwa nikisisitiza kwa washambuliaji kutofanya mzaha na nafasi tunazopata.

“Bado nina imani nao kubwa, ninaamini watafanya vizuri baadaye. Lakini sasa acha tuendelee kufanya kazi kwa ajili ya kuleta mabadiliko zaidi,” alisema Brandts.

Kocha huyo amegeuza uchezaji wa Yanga kwa kiasi kikubwa na hasa uchezaji wa kasi na pasi za uhakika, hali inayofanya kila kikosi kinachokutana na Yanga kuwa katika wakati mgumu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic