MALINZI NA TENGA...
Sekretarieti ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
imepokea barua ya Serikali ikielezea uamuzi wa Waziri wa Habari, Vijana,
Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara kutengua uamuzi wa Msajili wa Klabu
na Vyama vya Michezo nchini kuidhinisha marekebisho ya Katiba ya TFF toleo la
2012.
Baada ya kupokea barua hiyo jana alasiri (Februari 25 mwaka
huu), Sekretarieti iliwasiliana na Rais wa TFF, Leodegar Tenga ambaye ameagiza
kuitishwa kikao cha dharura cha Kamati ya Utendaji kujadili tamko hilo.
Kikao hicho cha Kamati ya Utendaji ya TFF kitafanyika
Jumamosi (Machi 2 mwaka huu) jijini Dar es Salaam.
0 COMMENTS:
Post a Comment