KATIBU MKUU TFF, ANGETILE OSIAH
Mwamuzi Msaidizi wa FIFA, Ferdinand Chacha ameondolewa
kuchezesha mechi za VPL baada ya kupata alama za chini kwenye mechi kati ya
African Lyon na Simba iliyochezwa mwezi uliopita Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam. Waamuzi wanaopata alama 6.5 au chini ya hapo kati ya 10 zinazohitajika
pia wanaondolewa kwenye mechi za VPL na FDL.
Waamuzi wengine walioondolewa kwa kutomudu mechi
walizochezesha za VPL ni Mathew Akrama (Yanga vs Simba), Ephrony Ndissa (Yanga
vs Simba), Ronald Swai (Yanga vs Mtibwa Sugar).
Walioondolewa kwa kupata alama za chini ni Alex Mahagi
(Simba vs JKT Ruvu), Methusela Musebula (Toto Africans vs Coastal Union),
Lingstone Lwiza (Toto Africans vs Coastal Union), Idd Mikongoti (Toto Africans
vs Mtibwa Sugar) na Samson Kobe (Toto Africans vs Mtibwa Sugar).
Masoud Mkelemi aliyekuwa mwamuzi wa mezani katika mechi ya
FDL kati ya Moro United na Villa Squad ameondolewa kwa kutofika kwenye mkutano
wa maandalizi ya mechi (Pre-match meeting) na alichelewa kwa dakika tano kufika
uwanjani.
0 COMMENTS:
Post a Comment