March 8, 2013



Unapokwenda katika mazoezi ya timu za soka kuna raha yake, pamoja na soka lakini wachezaji hawaishi vituko ambavyo ni burudani inayojitegemea tofauti na uwezo wanaouonyesha uwanjani.

Pamoja na kucheza mazoezi yao kwa juhudi au kuwavutia mashabiki wanaojitokeza kutokana na ushindani, lakini wamekuwa na maneno mengi utafikiri wanaigiza michezo ya kuchekesha.


Mfano, katika mazoezi ya Yanga wiki, moja ya vituko vilivyojitokeza ni kiungo nyota wa timu hiyo, Athumani Iddi ‘Chuji’ kushauriwa pamoja na kutokuwa na nywele katikati ya kichwa chake, eti anyoe kiduku.

Kiduku ni staili ya kuachia nywele katikati ya kichwa kama ambavyo hufanya mshambuliaji wa AC Milan, Mario Balotelli.

Wachezaji wawili wa Yanga, beki Mbuyu Twite na winga, Simon Msuva wana kiduku.
Hivyo wachezaji wenzake waliendelea kumtania Chuji wakimshauri anyoe kiduku, pamoja na kwamba anajulikana kwa ubabe, Chuji aliendelea kucheka akionyesha kudharau alichokuwa anaambiwa.

Kawaida amekuwa akinyoa nywele zake kuficha ‘walaza’ wake, lakini hivi karibuni, Chuji ameamua kuachia nywele hizo na sasa unaonekana vizuri kabisa huku akisisitiza kwamba yeye sasa ni mkongwe, hivyo haitaji kunyoa ‘unga’, yaani kipara  kila wakati.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic