March 8, 2013



Aliyekuwa Kocha Mkuu wa Simba, Milovan Cirkovic aliapa wakati anaondoka na kusema maneno ambayo huenda sasa yanaanza kuonekana taratibu.

Milovan raia wa Serbia ambaye alitupiwa zigo kubwa la lawama na viongozi wa Simba, kwamba ndiyo chanzo cha kuporomoka kwa Simba, alitoa maneno ambayo dalili zake zinaanza kuonekana sasa.


Milovan alisema anachojua viongozi wamekuwa tatizo kubwa sana wakati akiwa mwalimu na alivumilia mambo mengi sana.

Alisema alivumilia mambo mengi ikiwa ni pamoja na kunyamaza hata alipolazimishwa kuwachezesha wachezaji fulani.

Akasema viongozi wengi wa Simba, wamekuwa na tabia ya kuamini wanajua sana soka bila hata ya kulisomea, yeye amekwenda shule miaka 11 kusomea mchezo huo. Lakini bado walitaka kumfundisha nani acheze na nani abaki benchi.

Siku alipokuwa anaondoka, aliwaachia ujumbe mara mbili. Kwanza akasema hivi: “Kuwa na fedha si kujua soka.”
Halafu ujumbe wa pili akasema hivi: “Sipendi malumbano, ila nakuhakikishia muda ndiyo utakaosema kama kweli mimi ndiyo nilikuwa tatizo au wao, tusubiri.”

Sasa tayari Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili, Zacharia Hans Pope amejiuzulu na ndiye alikuwa jembe la usajili la Simba msimu huu.
Pia Makamu Mwenyekiti, Geofrey Nyanga ‘Kaburu’ ambaye pamoja na lawama nyingi pia alikuwa na msaada wake mkubwa Simba, ameachia ngazi jana, saa chache baada ya Hans Pope kuwa amebwaga manyaga.

Hapo ndipo pa kujiuliza, aliyoyasema Milovan ambaye alirejea Dar na kuanza kusumbukia malipo yake, ndiyo yameanza kutimia?

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic