March 8, 2013




MALKIA wa Nyuki ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ushindi ya Simba ambayo itahakikisha timu hiyo inafanya vizuri katika mechi zilizobaki.

Malkia wa Nyuki ambaye jina lake halisi ni Rahma Al Kharusi, amekuwa msaada mkubwa kwa Simba katika siku za hivi karibuni ingawa inaonekana anaangushwa kutokana na kutokuwa na utulivu na uongozi kuyumba ndani ya klabu hiyo.



Kamati hiyo iliyoteuliwa juzi kwenye hoteli ya Serana jijini Dar es Salaam tayari imeanza kumomonyoka baada ya aliyekuwa ameteuliwa kuwa makamu wa kamati, Geofrey Nyange Kaburu kutangaza kujiuzulu nafasi ya Umakamu Mwenyekiti wa Simba, sambamba na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili, Zacharia Hans Pope, jana. 

Akizungumza kuhusiana na kamti hiyo, Malkia wa Nyuki alisema lengo lao nmi kurudisha ushirikiano na kuisaidia Simba kucheza vizuri na kushinda mechi zilizobaki za ligi.

“Utaona kama watu wamekata tama, lakini sisi bado tunaamini kuna kila sababu ya kuangalia uwezekano wa kufanya vizuri katika mechi zilizobaki.
“Simba inaweza isiwe na nafasi, lakini ni timu yenye heshima zake. Inahitaji ushindi kwa ajili ya kuendelea kuonyesha ni timu kubwa.

“Lakini kingine ni kuepuka kuwaumiza wanachama na mashabiki wanaoiunga mkono. Kuna mengi ya kufanya, huenda vingine tukavifanya msimu ujao lakini suala la kushinda mechi zilizobaki ni muhimu sana,” alisema.




Wengine walioteuliwa katika kamati hiyo ni Katibu Joseph Itang’are ‘Kinesi’, wakati wajumbe ni Zacharia Hans Poppe, Swedi Nkwabi na Musley Al Rawah.

 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic