Baada
ya kupoteza mechi ya kwanza kwa kufungwa mabao 3-0 mjini Zanzibar, Jamhuri
ikiwa ugenini leo imelala kwa mabao 5-0 dhidi ya St George.
Katika
mechi hiyo iliyochezwa kwenye uwanja wa Taifa wa Addis Ababa, wenyeji ndiyo
walionekana kutawala mchezo muda mwingi.
Kwa
matokeo hayo, maana yake Jamhuri wameaga kwa jumla ya mabao 8-0 na kuendeleza
wimbi la timu za Tanzania kuishia katika hatua za awali.
0 COMMENTS:
Post a Comment