Huku ikionekana
kama itaamka, Arsenal ilijikuta ikilala kwa mabao 2-1 katika mechi ya
Premiership, leo.
Mechi hiyo
kubwa zaidi kwa Arsenal kwa maana ya utani wa jadi na Tottenham Hotspur ilikuwa
nzuri na ya kuvutia kutokana na timu zote kucheza mchezo wa kasi.
Lakini Bale na
Lennon ndiyo waliipatia mabao Spurs na mkongwe wa Kijerumani, Per Mertesacker akaifungia bao pekee. Kwa ushindi
huo Spurs imesogea hadi nafasi ya tatu ikiwa na pointi 54, nyuma ya Man City
katika nafasi ya pili na 56, huku vinara Man United wakiwa na 71.
Arsenal,
maarufu kama vijana wa Wenger wanabaki katika nafasi ya tano wakiwa na pointi
47, wakijaribu kupambana kuwavuka Chelsea wenye 51.
Kituko kingine
kilichotokea katika mechi ya leo ni shabiki wa Arsenal kumrushia Bale ganda la
ndizi ikiwa ni dalili ya ubaguzi wa rangi au kumfananisha mchezaji huyo na
nyani au sokwe.
Kidogo,
imeonekana si kitu cha kawaida kwa kuwa mashabiki wazungu hufanya hivyo kwa
wachezaji weusi au wale wenye asili ya Afrika.
KESHO JUMATATU:
Aston Villa Vs Man City
KESHO JUMATATU:
Aston Villa Vs Man City
0 COMMENTS:
Post a Comment