Ingawa Kocha Mkuu wa Man United,
Alex Ferguson alipinga kauli ya Roberto Mancini wa Man City kwamba timu yake
ina bahati kuwa kileleni, lakini amekubali kuwa Real Madrid inamuweka roho juu.
Man United itacheza na Real
Madrid katika mechi ya marudiano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya mechi
ya kwanza jijini Madrid kumalizika kwa
sare ya bao 1-1.
Kikosi cha United zaidi
kinawategemea washambuliaji wawili, Robin van Persie anayeonekana yuko katika
kiwango kizuri zaidi pamoja na Wayne Rooney ambaye pia anaonekana kuhofiwa
zaidi na Madrid.
Ferguson raia wa Scotland amesema
kasi ya Real Madrid hasa katika ushambuliaji wa kushitukiza au kaunta atak, ni
hatari sana na wachezaji wake Cristiano Ronaldo, Mesut Ozil na Angel Di Maria
ni hatari sana.
“Nilikwenda kushuhudia, Madrid ni
hatari sana wakati wanaposhambulia kwa kushitukiza, wachezaji wake hao watatu
ni hatari sana.
“Lakini ni suala la kulifanyia
kazi na mambo yanaweza kufanya kazi. Hatupaswi kuogopa, badala yake tahadhari
na mipango,” alisema Ferguson leo asubuhi.
Ferguson alikuwa kwenye Uwanja wa
Camp Noun a kuihuhudia Barcelona ikiteseka dhidi ya Real Madrid na kulala kwa
mabao 3-1.
Kila timu inaendelea na
maandalizi ya mchezo huo ambao utakuwa moja ya mechi gumzo zinazosubiriwa kwa
hamu na mashabiki wa soka.
angechezesha Web walaa wangekuwa na uhakika na ushindi ila duuu sie yeye
ReplyDelete