Matajiri wa jiji la Paris, klabu
ya PSG wameamua kufanya kufuru ili wamnase kiungo nyota wa Man City, Samir
Nasri.
PSG waliingia vitani kumuwania
Nasri mwaka 2011, lakini wakakwama baada ya kupigwa bao na Man City ambao walilipa
mamilioni ya pauni kwa Arsenal na kumchukua.
Taarifa kutoka ndani ya Man City
zimeeleza, Mkurugenzi wa ufundi wa PSG, Leonardo anavutiwa zaidi na Nasri na
yuko tayari kuishawishi klabu hiyo kutoa hadi pauni milioni 24 kumnasa.
Pamoja na hivyo, mshahara wa
Nasri ambao ni pauni 170,000 kwa wiki, hauwezi kuwa tatizo kwa mamilionea hao
wa Ufaransa wenye wachezaji ghali na maarufu kama David Beckham na Zlatan
Ibrahimovic.
Siku za hivi karibuni, Nasri
amekuwa katika uhusiano mbaya na kocha wake, Roberto Mancini raia wa Italia
ambaye aliamua kumshambulia Mfaransa huyo katika vyombo vya habari kwamba
haridhishwi na kiwango chake.
Kitu kimeonyesha kumchanganya
Nasri na PSG wameona ndiyo wakati mwafaka wa kumng’oa, ingawa uamuzi wa mwisho
utaendelea kubaki kwake Nasri mara baada ya msimu huu kwisha.
mchezaji yeyote akiondoka ilhali mzee wenger hakupenda basi huaga hafanikiwi yupo wapi flamin, jembe Jose antonio reyes,
ReplyDelete