Mabingwa wa Hispania, Real Madrid wametua jijini Manchester
na mshambuliaji wake, Cristiano Ronaldo na Kocha, Jose Mourinho wamekuwa
kivutio kikubwa.
Mashabiki wengiw aliojitokeza uwanja wa ndege walionyesha
wazi walitaka kuwaona watuw awili tu, Ronaldo na Mourinho ambao walishangiliwa
kwa nguvu wakati wakipita kuingia kwenye basi.
Ronaldo ambaye amekuwa akihusishwa na taarifa za kurejea Man
United ambayo ni klabu yake ya zamani alishangiliwa zaidi ikiwa ni dalili za
kukaribishwa tena katika klabu hiyo. Mashabiki hao walionyesha kutojali kwamba
Ronaldo atakuwa na kazi ya kupambana na klabu yao kesho usiku.
Madrid ambayo iko nchini humo kupambana na Man United katika
mechi ya marudiano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya 16 Bora baada ya sare ya
bao 1-1 jijini Madrid.
Tayari Madrid wameanza mazoezi na wamekuwa wakifanya katika
uwanja wa Etihad unaomilikiwa na wapinzani wakubwa we Man United, Manchester
City.
Imeelezwa Old Trafford hauko katika hali nzuri, hivyo ulikuwa
ukifanyiwa matengenezo kabla ya mechi ya kesho ambayo inasubiriwa kwa hamu
baada ya Madrid kuonyesha iko katika kiwango cha juu kwa kuwafunga wababe wa
Man United, Barcelona mara mbili mfululizo ndani ya siku nane.
0 COMMENTS:
Post a Comment