Naibu
Waziri we Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makalla amesema Katibu
Mkuu wa TFF, Angetile Osiah ana matatizo.
Akizungumza
jijini Dar es Salaam, Makalla alisema ana wasiwasi na maamuzi anayochukua Osiah
kama yanaweza kuchukuliwa na mtu aliyetulia.
“Sidhani
kama Angetile ni mzima vizuri, hivi karibuni nilikaa naye katika vikao kadhaa,
kuna wakati nililazimika kumuokoa kutokana na maamuzi aliyokuwa anachukua.
“Mfano sasa anasema hana imani na mimi, lakini tulipozungumza na Tenga akasema tofauti. Ninaamini uamuzi wa Tenga ndiyo sahihi,” alisema Makalla.
“Hata
kama watakuja wizarani kuzungumza, watanikuta mimi kwa kuwa waziri hatakuwepo
nchini kwa siku kumi. Mimi ndiyo watanikuta.”
Jana
TFF ilieleza kutokuwa na imani na Makalla kuhusiana na suala katiba yao mpya kukataliwa
na serikali kutaka waitumie ile ya mwaka 2006.
Hivyo
TFF, ikaomba itakapokwenda wizarani kuzungumza na serikali, Makalla
asiyehusishwe na badala yake wazungumza waziri mwenyewe Dk Fenella Mukangara.
0 COMMENTS:
Post a Comment