Yanga iliendelea na mazoezi leo
kwenye Uwanja wa Bora, Kijitonyama jijini Dare s Salaam chini ya kocha wake,
Ernie Brandts.
Mazoezi hayo yaliyochukua zaidi ya
saa mbili yalikuwa ni kupasha misuli na baada ya hapo wachezaji walipiga full
game ambayo inafanana kabisa na mchezo wa ligi kuu.
Wachezaji hao walionyesha kupania
ushindi, timu ya kijani ikitaka kuishinda ya njano. Mabeki walionyesha kukamia
kutotaka kupitwa.
Lakini mwisho, timu ya njano
iliyokuwa na ngome inayoongozwa na Kelvin Yondani na Mbuyu Twite ilijikuta
ikiachia mabao 3-1.
0 COMMENTS:
Post a Comment