Baada ya kucheza mechi yake ya 28 msimu huu dhidi ya
Norwich, wababe Man United wamefikisha mechi 800 za Ligi Kuu England.
Rekodi hiyo ya Man United inaunganishwa na timu nyingine
zilizokuwa katika ligi hiyo kuanzia msimu wa 1992-93 bila kuteremka daraja.
Katika mechi
hizo 800, Man United imeonyesha imekuwa na kikosi imara kwa muda mrefu, kwani
pamoja na kushinda mataji 12, lakini imefanikiwa kushinda mechi 522 ambayo ni
karibu ya robo tatu ya mechi zake.
Imeshinda
mataji hayo 12 ndani ya misimu 20 na kocha wake, Alex Ferguson ndiye kocha
aliyekuwa kwenye ligi hiyo tokea msimu huo na kuiongoza timu yake kushinda mabao
1,605 huku akiwa na beki iliyofungwa mabao 691 tu.
Arsenal imekuwa ya pili, ikiwa imeshinda ubingwa
mara tatu chini ya Wenger, Chelsea ya tatu ikiwa na vikombe kibao ingawa vitatu
ndiyo vya Premiership.
Liverpool
inashika nafasi ya nne ikiwa chini ya Chelsea
na Arsenal ingawa kihistoria inaonekana ni klabu kubwa zaidi. Nyingine zenye
mafanikio zaidi ni Tottenham Hotspur, Aston Villa na Everton.
0 COMMENTS:
Post a Comment