Shirikisho la Soka Tanzania
(TFF) limewasilisha rasmi maombi ya kuonana na Waziri wa Habari, Vijana,
Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara ili kuzungumzia uamuzi wake wa
kutengua usajili wa katiba ya 2012.
Maombi hayo
yaliwasilishwa rasmi Wizarani jana (Machi 4 mwaka huu) ambapo TFF imependekeza
kikao hicho kifanyike keshokutwa (Machi 7 mwaka huu) au Machi 13 mwaka huu.
Kamati ya Utendaji
ya TFF iliyokutana Machi 2 mwaka huu kujadili tamko ya Waziri kutengua matumizi
ya Katiba ya 2012 ndiyo iliyopendekeza kikao hicho kwa lengo la kusikiliza
upande wa TFF katika suala hilo.
0 COMMENTS:
Post a Comment