Unaweza kusema utakapofikia wakati wa
mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kati ya Man United na wageni wao Real Madrid
itakapoanza dunia ‘itasimama’, bei za tiketi zinaonekana kuwa tatizo.
Watu kadhaa ambao walinunua tiketi
za mechi hizo mapema, wamefikia kuuza hadi pauni 1,000 (zaidi ya Sh milioni
2.4).
Watu kadhaa walionekana karimu na
Uwanja wa Old Trafford jijini Manchester wakiwa wamebandika mabango kuwa
wanataka tiketi.
Baadhi ya mitandao pia ilikuwa
ikitangaa kuhusiana na tiketi hizo zinazolanguliwa na watu waliendelea
kuzinunua kutaka kuona kazi ya leo usiku kati ya Alex Ferguson dhidi ya Jose
Mourinho.
Mtandao wa ticket4football.com ulieleza
wazi kuhusiana na mauzo ya tiketi na watu wakaonekana kugombea.
Asilimia kubwa ya mashabiki jijini
Manchester wanataka kuona Ronaldo anataka kufanya vipi kazi yake leo usiku na
kama ataweza kuikomboa Madrid ambayo katika mechi ya kwanza ikiwa nyumbani
ililazimishwa sare ya bao 1-1.
Tiketi ambazo ziliuzwa halali
kuanzia pauni 250, baadaye zilipanda haraka hadi kufikia pauni 750. Lakini hali
inazidi kuonekana mbaya, kwani kadiri muda unavyosonga mbele huenda zikavuka
zaidi ya pauni 1000.
0 COMMENTS:
Post a Comment