March 2, 2013




Mshambuliaji wa AC Milan, Kevin-Prince Boateng na Rais wa Fifa, Sepp Blatter watakutana mwezi huu mwishoni kujadili kuhusiana na suala la ubaguzi wa rangi.

Fifa imetoa taarifa ya kuwepo kikao kati ya Boateng raia wa Ghana pamoja na Boateng na tayari kimepangwa kufanyika Machi 22 jijini Zurich, Uswiss.

Boateng amekuwa mpiganaji mkubwa wa masuala ya ubaguzi, Januari mwaka huu aliwaongoza wachezaji wenzake wa AC Milan wakiwa uwanjani kulaani kuhusiana na vitendo hivyo vya ubaguzi wa rangi.
 
Boateng amealikwa katika moja ya vikao vya Umoja wa Taifa (UN) kuhusiana na kupinga masuala ya ubaguzi wa rangi.
Tayari Blatter ameshazungumza kwenye vyombo vya habari na kumsifia Boateng kutokana na alichokionyesha kuhusiana na suala hilo ambalo limekuwa likichukua kasi kubwa hasa barani Ulaya.


Ubaguzi wa rangi umekuwa tatizo kubwa kuanzia uwanjani hadi kwa mashabiki ambao wamekuwa wakiwazomea wachezaji weusi kwa kutumia ndizi au mifano ya masokwe.

Mbaya zaidi, umefikia wakati hadi waamuzi wamekuwa wakilaumiwa kuhusiana na suala hilo hali inayowafanya wachezaji weusi kuwa katika hali ya wasiwasi.


Hata hivyo, Fifa ambayo inahusika na soka duniani kote, imekuwa ikifanya juhudi za dhati kupambana na suala hilo ambalo linaonekana kuwa na nguvu kubwa katika nchi za Ulaya Mashariki ambao pamoja na kuwa ndiyo masikini zaidi barani humo, lakini wamekuwa wajeuri na wanaongoza kwa tabia hizo chafu na za kipuuzi za ubaguzi wa rangi.
 

 



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic