Villa wakati wakiwa Ligi Kuu Bara...sasa wanawania kurejea.
Michuano ya Ligi Daraja la Kwanza Tanzania
(FDL) inaendelea kesho (Machi 2 mwaka huu) katika makundi yote matatu. Villa
Squad itaivaa Ashanti United kwenye Uwanja wa Karume, Dar es Salaam katika moja
ya mechi za kundi B.
Kundi A ni mechi kati ya Kurugenzi ya
Mafinga dhidi ya Mbeya City wakati Polisi Iringa vs JKT Mlale, na Majimaji vs
Mkamba Rangers zilizokuwa zicheze kesho (Machi 2 mwaka huu), sasa zitaumana
Machi 3 mwaka huu mjini Iringa na mjini Songea.
Upande wa kundi B kesho (Machi 2 mwaka
huu) ni Green Warriors vs Transit Camp (Mlandizi) wakati keshokutwa (Machi 3
mwaka huu) Polisi Dar vs Tessema (Karume) na Ndanda vs Moro United katika
Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.
Mechi za kundi C kesho ni JKT Kanembwa
vs Polisi Tabora (Lake Tanganyika), Polisi Mara vs Polisi Dodoma (Karume,
Musoma), Morani vs Pamba (Kiteto) na Mwadui vs Rhino Rangers (Kambarage,
Shinyanga).
0 COMMENTS:
Post a Comment