April 16, 2013





Kocha Mkuu wa Kenya, Adel Amrouche amewaonya Azam FC kuhusiana na uchezaji wa FAR Rabat.

Azam FC inawakaribisha FAR Rabat ya Morocco katika mechi ya Kombe la Caf, Jumamosi kwenye Uwanja we Taifa, Dar.
Amrouche ambaye ana uzoefu mkubwa na soka la Afrika Kaskazini kwa kuwa asili yake ni Algeria, amesema Wamorocco hasa upande wa klabu ni wepesi sana kwa kushambulia haraka.

“Wanachotakiwa Azam FC ni kucheza mpira wa kasi, kama watashindwa na kuiga wanachotaka wao basi watapotea.


“Kingine kwa kuwa Azam wanaanzia nyumbani, basi ni lazima wacheze na kuhakikisha wanashinda mabao angalau matatu ili kujiweka katika nafasi nzuri,” alisema Amrouche ambaye pia ana uzoefu na soka la ukanda wa Afrika Mashariki na Kati kwa kuwa amewahi kufanya kazi DR Congo, Burundi na sasa Kenya.

kwa mujibu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), FAR Rabat wanatarajiwa kuwasili nchini kesho.

AS FAR KUWASILI KESHO KUIKABILI AZAM
Wapinzani wa Azam katika michuano ya Kombe la Shirikisho, AS FAR Rabat ya Morocco wanatarajiwa kutua nchini kesho (Aprili 17 mwaka huu) saa 7 mchana kwa ndege ya Emirates.

Msafara wa timu hiyo wenye watu 28 utafikia hoteli ya Sapphire iliyoko maeneo ya Kariakoo, Dar es Salaam tayari kwa mechi hiyo ya kwanza ya raundi ya pili itakayochezwa Jumamosi (Aprili 20 mwaka huu) saa 10 kamili jioni Uwanja wa Taifa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic