April 16, 2013





Ujumbe wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) tayari uko nchini na umeanza kazi yake.
Ujumbe huo chini ya Mkuu wa Idara ya Uanachama wa Fifa, Primo Corvaro umewasili jana nchini tayari kutatua mgogoro wa Uchaguzi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

Msemaji wa TFF, Boniface Wambura amesema Primo ameongozana na Mkuu wa Kanda hii, Ashford Mamelodi.
“Wakiwa hapa watawendelea na shughuli yao lakini wakiweza watakutana na Waziri mwenye dhamana ya michezo.

“Walijaribu kukutana naye leo lakini ikashindikana kwa kuwa waziri yuko bungeni amebanwa na majukumu mengine.
“Watajitahidi kukutana naye lakini kama itashindikana basi, haina maana ni lazima wafanye hivyo lakini wanakwenda kwa nia ya kwenda kumsalimia tu,” alisema Wambura.

Hata hivyo, Wambura amesema Ujumbe huo wa FIFA umeshindwa kukutana na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, D. Fenella Mukangara kwa kuwa hivi sasa yupo Bungeni, Dodoma.


Kazi kubwa ya Corvaro na Mamelodi watakutana na wagombea ambao wana malalamiko yao.
Wagombea watakaosikilizwa ni Jamal Malinzi nayegombea Urais  aliyepitishwa na Kamati ya Uchaguzi. Lakini akakatiwa rufani iliyopitishwa na Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF, akaondolewa kwenye mchakato wa uchaguzi.

Wengine watakaosikilizwa ni Mgombea wa nafasi ya Makamu wa Rais wa TFF, Michael Wambura ambaye alikatwa na Kamati ya Uchaguzi ya TFF na rufani yake kukataliwa na Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF.

Mgombea wa nafasi ya uenyekiti wa Bodi ya Ligi, Hamad Yahya aliyepitishwa na Kamati ya Uchaguzi, lakini mwekaji pingamizi akakata rufani ambayo ilikubaliwa na Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF na kuondolewa. Aliomba shauri lake liangaliwe upya, lakini Kamati ya Rufaa ya Uchaguzi ya TFF ikatupa ombi lake.

Mgombea wa nafasi ya ujumbe wa Kamati ya Utendaji, Farid Salim Mbaraka  ambaye alienguliwa na Kamati ya Uchaguzi na baadaye rufani yake kwa Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF kutupwa na hali kadhalika ombi lake la kutaka shauri lake liangaliwe upya, kukataliwa.




RATIBA YA UJUMBE WA FIFA NCHINI
Tarehe /Muda
Tukio
15 Aprili 2013
Saa 12:30 – 03:00
Kuwasili kwa wajumbe wa FIFA
15 Aprili 2013
Saa 04:00 – saa 05:00 usiku
Kikao na Rais wa TFF pamoja na Sekretarieti
16 Aprili 2013
Saa 05:30 – 06:30 asubuhi
Kukutana na Kamati ya Uchaguzi ya TFF kupata taarifa ya uchaguzi
16 Aprili 2013
Saa 06:30 – 08:00 mchana
Chakula cha Mchana
16 Aprili 2013
Saa 08:00 – 12:00 jioni
Kukutana na wagombea walioondolewa
17Aprili 2013
Saa 03:00 – 05:00 asubuhi
Kukutana na Kamati ya Rufaa za Uchaguzi ya TFF
17 Aprili 2013
Saa 05:30 – 06:30
Mchana
Kupewa taarifa zinazohusiana na mchakato wa uchaguzi, i.e., kesi zilizo mahakamani
17 Aprili 2013
Saa 08:00 – 10:00 jioni
Kukutana na watu wengine ambao FIFA wanaweza kuomba kukutana nao
17Aprili 2013
Saa 10:30 – 11:00 jioni
Mkutano na waandishi wa habari – kushukuru mamlaka na pande zilizohusika kwa ushirikiano
18 Aprili 2013
Saa 10:00 – 12:00 Alfajiri
Kuondoka hotelini kwa ajili ya safari

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic