April 16, 2013



 
Hii ndiyo ilikuwa picha ya kuvutia zaidi katika mechi kati ya Simba dhidi ya Azam kwenye Uwanja wa Taifa Jumapili iliyopita.
Inaonekana Humprey Mieno ‘Hum’ raia wa Kenya akijaribu kumpokonya mpira kinda wa Simba, Abdallah Seseme bila ya mafanikio, lakini kabari aliyompiga ndiyo kivutio zaidi.


Kiasi fulani mwamuzi, Oden Mbaga aliuchuna lakini akaona Mieno anaweza kuua, hivyo akalazimika kupiga filimbi.

Mechi hiyo ya kuvutia ilimalizika kwa sare ya mabao 2-2, Simba ikitangulia kufunga yote mawili katika kipindi cha kwanza na Azam FC ikasawazisha katika kipindi cha pili.

PICHA NA CHAMPIONI NEWSPAPER

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic