April 24, 2013



Abdul (kulia) akiwa na Luhende naTelela..

Beki wa kulia wa Yanga, Juma Abdul amelazimika kuendelea kubaki nje katika kikosi cha Yanga kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya goti.
Abdul aliyejiunga na Yanga akitokea Mtibwa Sugar msimu huu, anaendelea na matibabu.

Kwa mujibu wa daktari wa Yanga, Nassor Matuzya, beki huyo huenda akaanza mazoezi mepesi kesho.

“Matibabu yanakwenda vizuri na kama kila kitu kitaenda kama tulivyopanga, basi huenda kesho asubuhi akaanza mazoezi,” alisema Matuzya.
 
Kavumbagu...
Pamoja na Abdul, mshambuliaji Didier Kavumbagu jana alianza mazoezi maalum wakati kikosi cha Yanga kinajifua kwenye Uwanja wa Loyola, Mabibo, Dar.

Wakati wenzake walikuwa wakifanya mazoezi pamoja, Kavumbagu alikuwa akikimbia taratibu na Matuzya alisema hiyo ni programu maalum.

Kavumbagu alikuwa anasumbuliwa na maumivu makali ya msuli kamba ambao ulimuweka nje kwa siku kadhaa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic