April 6, 2013




DK 89,90, Azam FC wanaendelea kupoteza nafasi za wazi, mwisho mechi inamalizika kwa sare ya bila kufungana. Maana yake Azam FC inasonga mbele kutokana na ushindi wake wa ugenini wa mabao 3-1.

Dk 83, Tchetche naye anapoteza nafasi ya wazi.


Dk 67, Bolou anakosa bao la wazi, alimpa pasi Mieno, naye akamrudishia, walinzi wa BYC wakadhani ameotoa, hivyo akasogea kabisa karibu na kipa, akiwa ndani ya 18 akitazamana na kipa, akaupaisha mpira..buuuuuu..

Dk 51, Faulo maridadi iliyopigwa na Mcha, mpira unamfikia Bocco, akiwa katika nafasi nzuri anajigonga miguu hadi mpira unatoka.


Dk 46, Azam wanamtoa Umonyi, nafasi yake inachukuliwa na Mcha.
 

MAPUMZIKO 0-0:
Dk 41, Mieno anachonga kona safi, inayotua kwa Atudo, anapiga kisigino saaafi, lakini mpira unagonga mwamba na kuokolea. 

Dk 33, Bocco anawatoka mabeki wa BYC, anatoa pasi nzuri kwa Mieno ambaye anaudokoa mpira unaompita kipa, lakini wakati ukielekea kuvuta mstari, anatokea beki na kuukoa.

Dk 26, BYC wanafanya shambulizi kali na mpira wa shuti la Barshal linapanguliwa na Mwadini na kuwa kona ambayo haikuwa na majibu.
Dk 11, Tchetche anawatoka mabeki wawili na kupiga krosi lakini mpira wa kichwa wa Umonyi unadakwa na kipa vizuri.

Mechi inaanza kwa mashambulizi ya zamu lakini kila timu haijatulia.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic