Sunzu akiwa katika mazoezi ya Bongo Movie, anamsikiliza kocha kwa umakini hasa... |
Siku tatu zilizopita,
Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Liewig alimtimua tena mazoezini mshambuliaji wake
Felix Sunzu.
Sunzu raia wa
Zambia alikwenda mazoezini kwenye Viwanja vya Leaders jijini Dar ili kufanya
mazoezi na ilielezwa aliruhusiwa na uongozi, lakini Liewig hakuwa na taarifa.
Hivyo
akaamuru Sunzu aondoke, bila ya hiyana Mzambia huyo akaondoka na kujiunga
mazoezi ya Bongo Movie yaliyokuwa kwenye uwanja wa vumbi hapohapo Leaders.
Sunzu bila
ya hiyana, akaendelea kujifua kwa nguvu na timu hiyo inayojumuisha wasanii wa
filamu tena kwa nidhamu ya hali ya juu.
Ukimuangalia
usoni alikuwa ni mtu anayetia huruma, Liewig ambaye alionekana wazi hakujisikia
vizuri kuona Sunzu akifanya mazoezi upande ule alianza kulalama.
Mara baada
ya mazoezi, Mfaransa huyo alianza kulalama kwamba amedharauliwa na hakupewa
taarifa huku akisisitiza hadi apate maelezo kutoka kwa Sunzu ndiyo atakubali
ajiunge na timu.
Upande wa pili, Simba walikuwa wanaendelea na mazoezi... |
Siku iliyofuata,
Msemaji wa Simba, Ezekiel Kamwaga akasema mchezaji huyo alitakiwa kuandika
barua ya kujieleza.
Sunzu
ameingia katika tafrani hilo baada ya kutoweka mazoezini bila ya taarifa na
kukaelezwa kwamba alikimbilia kwao Zambia lakini baadaye alidai alikuwa jijini
Dar amejichimbia tu kwake eneo la Keko.
Liewig analalama mara baada ya mazoezi kwisha, kulia ni Mwandishi wa Championi, Khatim Naheka 'Ntu'... |
0 COMMENTS:
Post a Comment