April 16, 2013


Akiwa na Fidel Castro...


Diego Maradona juzi aliamua kumtembelea Rais wa zamani wa Cuba, Fidel Castro nyumbani kwake mjini Havana.


Maradona ambaye alifunga mabao 34 katika mechi 91 alizoichezea timu ya taifa ya Argentina, alimtembelea rais huyo maarufu duniani kote na kufanya naye mazungumzo.

Picha mbalimbali kwenye vyombo vya habari zilimuonyesha Maradona akiwa anasalimiana na Castro huku wakiwa na furaha kubwa pamoja.
Maradona amekuwa rafiki mkubwa na mtu anayeunga mkono siasa za mfumo wa Castro ambaye ni mmoja wa wakomunisti ngangari.

Pamoja na kumtembelea Castro, Maradona alitua nchini Venezuala na kumuunga mkono mgombea wa urais aliyekuwa anaunga mkono siasa za marehemu Hugo Chavez ambaye alishinda uchaguzi huo.
 
Akiangana na Rais Maduro wa Venezuala..



Maradona alimtembelea na kushiriki katika kampeni za Nivolas Maduro, kabla ya uchaguzi huo ambao baadaye aliibuka mshindi.

Akiwa na Maduro, Maradona alimkabidhi jezi ya Argentina na kumuambia amfikishie salama za pole na msamaha kwa familia ya Chavez kwa kuwa alishindwa kuhudhuria mazishi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic