April 22, 2013



 
Baada ya kutojitambua kwa zaidi ya saa 24, hatimaye Dzhokhar Tsarnaev ameamka na kuanza kuhojiwa na maofisa wa usalama wa Marekani.

Maofisa hao wamekuwa wakimhoji Dzhokhar ,19, ambaye ni mtuhumiwa wa pili wa ulipuaji wa bomu la Boston Marathoni.


Kaka yake aliuwawa wakati akipambana na polisi, lakini Dzhokhar  ameamka na kuanza kuhojiwa kwa kutumia maandiko.


Maofisa wa polisi wamesema wamekuwa wakimhoji kwa kuandika naye anajibu.


Hata hivyo inaonekana bado hawajajua mambo mengi lakini amewaeleza kwamba hakutaka kukamatwa akiwa hai.
 
Tamerlan & Dzhokhar
Ndiyo maana aliweka bunduki katika mdomo wake na kujilipua akiwa na nia ya kujiua lakini hali haikwenda kama alivyotaka.
Wakati anakamatwa Dzhokhar  alikuwa amepoteza damu nyingi na sasa yuko katika hospitali moja mjini Boston ambako kuna ulinzi mkali sana.


Kaka yake Tamerlan ,26, aliuwawa wakati akipambana na polisi baada ya wawili hao kugundulika walihusika na ulipuaji wa  mabomu mawili siku ya mashindano ya Boston Marathon jijini Boston,

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic