April 22, 2013



 
Mtukutu na mbaguzi maarufu wa rangi, mshambuliaji Luis Suarez we Liverpool ameomba radhi kutokana na kitendo chake cha kumng'ata beki wa Chelsea, Branislav Ivanovic katika mechi yao ya Ligi Kuu England jana.

Katika mechi hiyo iliyomalizika kwa sare ya mabao 2-2, Suarez akiwa shujaa, lakini akaonyesha kitendo cha ajabu kwa kumg’ata mkononi beki huyo wakati wakiwania mpira.


Pamoja na Suarez kuomba radhi, lakini imegundulika ndiyo tabia yake na jana haikuwa mara ya kwanza kumng’ata mtu uwanjani.

Mwaka 2010 wakati akiicheea Ajax ya Uholanzi, alimng’ata mchezaji wa PSV Eindhoven, Otman Bakkal hadi alama za damu zikajitokeza katika jezi.
Baadhi ya mitandao imeanza kupendekeza kuanzishwa kwa sheria mpya ikiwa ni pamoja na kuwapa adhabu watu kama Suarez kucheza wakiwa wamezibwa midomo yao.


Baadhi ya picha zimeonyesha Suarez akiwa amezibwa kama mbwa wakorofi ili kuepusha wasiume watu.

Mitandao mingine imetania kwamba Suarez alikuwa ni mwenye njaa ndiyo maana kashindwa kujizuia na alipomuona Ivanovic alifikiri ameona bugger, hivyo akajisevia na kung’ata kwa juhudi kubwa.


Suarez haishi vituko kwani miezi kadhaa iliyopita alikumbana na adhabu ya faini ya pauni 40,000 na kusimamishwa kucheza mechi nane za Premiership baada ya kumfanyia vitendo vya kibaguzi beki wa Manchester United, Patrice Evra raia wa Ufaransa. 

Taarifa nyingine zilieleza kwamba Ivanovic ambaye huaminika ni mtaratibu, alizungumza na maofisa wa polisi wa Merseyside mara tu baada ya mechi, lakini hakutaka kufungua mashitaka au kwenda nje ya sheria za soka kuhusiana na suala hilo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic