Hali ya kiungo wa Yanga,
Haruna Niyonzima bado haijatengemaa vizuri.
Kiungo huyo leo
alilazimika kufanya mazoezi baada ya Kocha Ernie Brandts kufanya mazungumzo kwa
muda na daktari wa timu, Nassor Matuzya.
Baada ya mjadala huo,
Brandts aliruhusu afanye mazoezi lakini Dk Matuzya alilazimika kumuwekea plasta
kwenye pua yake ambayo ilionyesha ina jeraha.
Katika mechi ya Ligi Kuu
Bara dhidi ya Mugambo Shooting, Niyonzima alikaa benchi ingawa baada ya hali
kuwa ngumu akaingia na kusaidia kupatikana kwa bao la kusawazisha.
Mechi hiyo kwenye Uwanja
wa Mkwakwani mjini Tanga ilimalizika kwa sare ya mabao 1-1 na kupunguza kasi ya
Yanga ambayo inakwenda kasi kutwaa ubingwa.
0 COMMENTS:
Post a Comment