April 22, 2013



Kitendo cha mshambuliaji wa Liverpool kumuuma beki Branislav Ivanovic wa Chelsea kimeanza kuzua madhara kwa watoto barani Ulaya.

Mtoto mmoja amemuuma mwenzake walipokuwa wakipigana shuleni na mama wa mtoto aliyeng’atwa ametupa lawama moja kwa moja kwa Suarez.


Mama huyo amesema amepigiwa simu kutoka shuleni kwamba mwanaye ameng’atwa na mwenzake.

“Lakini mwalimu kaniambia tukio lilikuwa kama lile la Suarez na beki wa Chelsea,” alisema mama huyo alipozungumza na BBC 5Live.

Tayari watoto kadhaa wamekuwa wakionywa kutoiga tukio hilo la Suarez kwani linaweza kuwaletea madhara.

Tayari  Suarez amepigwa faini na Liverpool kutokana na kitendo hicho lakini hata FA imetangaza kumuadhibu na watu kadhaa wamekuwa wakilaani kitendo hicho kufanywa na mtu mzima kama yeye, tena baba wa mtoto mmoja.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic