April 10, 2013

Shirikisho la Soka Ulaya (Uefa) liko katika hatua ya mwisho kupitisha sheria mpya ambayo itakuwa ni kali kwa wabaguzi wa rangi katika mchezo wa soka.


Katibu Mkuu wa Uefa, Gianni Infantino amesema kupitia sheria hiyo mpya, wachezaji, mashabiki na hata viwanja vitakumbana na adhabu kali.
Alisema kiasi cha chini kabisa katika adhabu hiyo mpya kwa mchezaji itakuwa ni kufungiwa mechi kumi.

 “Ikiwa ni shabiki atabainika kufanya vitendo vya ubaguzi, mara moja atafungiwa kuingia katika uwanja ambao tukio lilitokea. Lakini bado kuna adhabu anaweza akakumbana nayo ambauo kwa uchache kabisa ni adhabu ya Euro 50,” alisema Gianni.


Wiki iliyopita, Rais wa Fifa, Sepp Blatter alisisitiza kuwepo kwa adhabu kali kwa wale wanaoendelea masuala ya ubaguzi wa rangi katika soka.

Msimu uliopita, John Terry  wa Chelsea alifungiwa mechi nne kutokana na vitendo vya ubaguzi wa rangi dhidi ya Antoni Ferdinand na Mruguay, Luis Suarez we Liverpool akafungiwa kucheza mechi nane kwa kumfanyia vitendo vya kibaguzi, Patrice Evra wa Manchester United.

Vitendo vya ubaguzi wa rangi vimekuwa vikichukua nafasi kila kukicha, wakati fulani Muitaliano Mario Balotelli alitishia kumuua mtu yoyote atakayemfanyia vitendo vya ubaguzi wa rangi, hata hivyo kauli hiyo haikusaidia kwani walimtupia ganda la ndizi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic