Borussia
Dortmund ya Ujerumani ndiyo timu inayoaminika kuwa na mashabiki wengi zaidi
wanaoyoiunga mkono na wamekuwa nayo bega kwa beka katika kila mechi.
Mafanikio yao
ya kufuzu hadi nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya tena katika dakika mbili
za mwisho imekuwa ni faraja kubwa kwa mashabiki wao.
Borussia
maarufu kama ukuta wa njano, wanatumia rangi za njano na nyeusi na kila mechi
inayowahusu, uwanja huonekana kuna rangi aina mbili tu. Hiyo inatokana na
mashabiki kujitokeza kwa wingi zaidi.
Katika mechi
yao ya jana dhidi ya Malaga, mashabiki hao waliingia uwanjani wakiwa na bango
maalum lenye picha ya mtu akiwa na darubini.
Bango hilo
limeelezwa kuwa bora na lenye mvuto zaidi kuliko yote ambayo yamewahi kuonekana
uwanjani.
Baadhi yamekuwa
yakiashiria ubabe, kama lile ambalo hutumiwa na mashabiki wa timu ya taifa ya
Urusi au lile wanalotumia mashabiki wa timu ya taifa ya Serbia.
Lile la
Borussia, linaonyesha amani tu lakini aliyeshika darubini anaonyesha ishara ya
kuwa wao wanamuona kila mtu na wamejiandaa na tayari pongezi zimemiminika kwa
waliolibuni.
0 COMMENTS:
Post a Comment