May 1, 2013



Kila mmoja alikuwa na lake la kusema, wengine walithubutu kutamka kuwa bora Real Madrid wamekufa kiume ingawa kipigo ni kipigo.

Barcelona wameaga michuano ya Ligi ya Mabingwa mwaka huu kwa aibu ambayo itabaki katika historia yao kwa kipindi kirefu baada ya kufungwa jumla ya mabao 7-0.


Mabao 4-0 mjini Munich na 3-0 ndani ya Camp Nou, ni aibu ya aina yake, mbaya zaidi wageni Bayern walionekana kuutawala zaidi mchezo.
Mabao ya Bayern yalifungwa na Robben, Pique akajifunga na Muller akamalizia la tatu.


Lionel Messi ambaye ni sawa na mkombozi alikuwa kwenye benchi akiishuhudia Barcelona ikiumizwa nyumbani na Wajerumani hao.

Mara kadhaa, Aarjen Roben na Frank Ribery wa Bayern ndiyo walionekana kuwa matatizo makubwa kwa beki ya Barcelona iliyoongozwa na Gerard Pique.



Wakati washambuliaji wa Barcelona walioongozwa na David Villa walikuwa wachovu na wasio tishio hata kidogo.

Ajabu Barcelona waliamua kuwatoa viungo wao tegemeo Iniesta na Xavi ikiwa ni dalili ya kukubali matokeo mapema.



Munich imesonga fainali, sasa inakutana na wapinzani wake wakubwa katika Bundesliga, Borussia Dortmund ambao wamewavua ubingwa hivi karibuni.

Dortmund walisonga baada ya kuitoa Real Madrid kwa jumla ya mabao 4-3 ikiwa walishinda kwao kwa mabao 4-1 na baadaye wakapoteza jana kwa kuchapwa 2-0.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic