May 1, 2013




Pamoja na Real Madrid kutolewa katika nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa jumla ya mabao 4-3, Cristiano Ronaldo amesema anabaki.

PSG na Man United zilionyesha nia ya kumtaka mshambuliaji huyo aliyetua Madrid akitokea Man United iliyomnasa akiwa kinda tokea Sporting Lisbon ya Ureno.

“Nina mkataba wa miaka miwili, sina hofu na ninaona nina furaha. Nitabaki kuendelea kupambana kupata makombe,” alisema Ronaldo.

Kauli hiyo inaonekana kuwa tata, bado haieleweki kama amesema akiwa amemaanisha kweli au baadaye ataondoka zake kutokana na taarifa za mwanzo zilizokuwa zikieleza anataka kurejea United.

Tayari Kocha Mourinho anaonekana ataondoka na kutua Chelsea, klabu yake ya zamani ambayo alifanya vizuri akiwa hapo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic