May 1, 2013



Kipigo cha jumla ya mabao 7-0 ilichotoa Bayern Munich kwa Barcelona ni kikubwa kuliko vyote vilivyowahi kutolewa katika Ligi ya Mabingwa hatua ya nusu fainali.

Bayern ilishinda kwa mabao 4-0 nyumbani na 0-3 ugenini, maana yake ndiyo ushindi mkubwa zaidi kuwahi kutokea katika michuano hiyo katika nusu fainali.

Barcelona ambao walikuwa nyumbani, walicheza kichovu na hawakuonyesha kama kweli wangeweza kurudisha mabao manne waliyofungwa na kufunga la tano.

Badala yake, wageni ndiyo walionekana kama wamepoteza mchezo wa kwanza na walitaka kufunga mabao mengine.

Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya sasa ni ya Wajerumani tupu na itachezwa Mei 25 kwenye Uwanja wa Wembley jijini London, England.

 Bayern inakutana na wapinzani wao Borussia Dortmund ambao wana hasira ya kupokonywa ubingwa wa Bundesliga.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic