May 1, 2013


Kiungo mshambuliaji wa Simba, Amri Kiemba amesema yupo tayari kurejea katika klabu ya zamani ya Yanga.

Kiemba anasema yuko tayari kusaini katika klabu yoyote inayoshiriki Ligi Ligi Kuu Tanzania Bara hata kama ni Yanga.

 

Mkataba wa Kiemba na Simba, unamalizika mara baada ya msimu huu ambao umebaki mechi mbili tu.

Maana yake Kiemba anaweza kuzungumza na timu yoyote kwa mujibu wa sheria za usajili za Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa).

Hivyo Yanga na timu nyingine zinaweza kuzungumza na kiungo huyo ambaye ameonyesha uwezo mkubwa hasa msimu huu.

Awali ilionekana kama Kiemba alikuwa amepoteza mwelekeo, lakini kutua Simba kwa Kocha, Milovan Cirkovic raia wa Serbia kulimrejesha katika kiwango cha juu.

Kiemba alicheza Yanga wakati ikiwa chini ya Kocha Jack Chamangwana raia wa Malawi. Lakini amewahi kukipiga Miembeni ya Zanzibar kabla ya kurejea Bara na kujiunga na Moro United.

 


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic