May 1, 2013



 Kocha Mkuu wa Yanga, Ernie Brandts amesema kikosi chake dhidi ya Coastasl Union kitawashangaza wengi leo.

Yanga inaivaa Coastal leo saa 10 jioni katika mechi ya Ligi Kuu Bara ambayo itakuwa ni ya pili kutoka mwisho kwa Yanga. Baada ya mechi hiyo ifatunga msimu na Simba.

Tayari Yanga ni mabingwa baada ya Coastal Union kutoka sare ya Azam FC mjini Tanga wiki iliyopita.

Brandts alisema mechi hiyo atatoa nafasi kwa wachezaji kadhaa ambao hawajawahi kupata nafasi.

“Njoo uone, kutakuwa na mabadiliko makubwa na kikosi kitawashangaza wengi,” alisema.

Kabla ya hapo, msemaji wa Yanga, Baraka Kizuguto aliiambia Salehjembe kwamba uwanjani kutakuwa na ‘sapraiz’.

“Njooni muone, ni bonge la sapraiz,” alisema Kizuguto.

Brandts anategemea kuwapumzisha wachezaji wake sita ambao wana kadi za njano ambao ni pamoja na kipa, Ally Mustapha ‘Barthez’, Athuman Idd ‘Chuji’, Simon Msuva, David Luhende, Didier Kavumbagu, Hamis Kiiza ili kuepuka wasiikose mechi ya Simba kama watalambwa kadi nyingine ya njano ambayo itakuwa ya tatu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic