May 14, 2013



  Roberto Mancini amefukuzwa kazi siku moja baada ya kutimiza mwaka mmoja baada ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu England.

Kutokana na kufukuzwa huko katika mtindo ulioonekana ni wa kikatili, Mancini atalipwa pauni milioni 7 kwa kuwa mkataba wake na klabu hiyo ulikuwa na miaka mitatu mbele.


Mancini raia wa Italia ameiwezesha Manchester City kutwaa Kombe la Ligi Kuu England na lile maarufu la FA.

Kocha huyo alipata taarifa za kufutwa kwake kazi dakika chache baada ya kutoka mazoezini kujiandaa na mechi dhidi ya Reading. Mmoja wa Wakurugenzi, Ferran Soriano ndiye alimueleza lakini ikaelezwa baadaye akazungumza na bosi mwenye timu, Mwenyekiti Khaldoon Al Mubarak ambaye yuko Abu Dhabi.


Taarifa zinaeleza, tajiri huyo mwarabu hakupenda kumfukuza Mancini lakini baada ya kufungwa katika fainali ya Kombe FA kwa bao 1-0 na Wigan, asilimia kubwa ya wakurugenzi walitaka aondolewe.

Pellegrini, 59, ndiye anaonekana ni chaguo la Man City ingawa tayari kocha huyo amezungumza kwamba hana mpango huo.
Imeelezwa kumekuwa na taarifa za kutaka kujiunga na Barcelona ambayo ina hofu na afya ya kocha wake, Tito Vilanova anayetibiwa ugonjwa wa kansa.


Tayari Man City wako tayari kumtwaa kwa Pellegrini kutoka Malaga kwa kulipa pauni milioni 3.3 ili kuvunja mkataba wake na mazungumzo yamekuwa yakiendelea.


Baada ya kutimuliwa kwa kocha huyo aliyekuwa mshindani mkubwa wa Alex Ferguson, mashabiki wa Man United walionekana mtaani wakiwa na mapango yaliyokuwa yenye maandishi yanayotaka “akapumzike kwa amani” huku kukiwa na picha za Ferguson kuonyesha wanamkubali zaidi.
 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic