May 19, 2013



 
Baada ya kuifunga Simba kwa mabao 2-0, Kocha Mkuu wa Yanga, Ernie Brandts anatarajia kuondoka leo kwenda kwoa Uholanzi.

Brandts anakwenda Uholanzi kwa mapumziko baada ya msimu wa Ligi Kuu Bara kufikia tamati.

Kocha huyo ameiambia Salehjembe kwamba atakaa Uholanzi kwa wiki kadhaa kablaya kufanya safari ya mapumziko nje ya nchi hiyo.

“Nitakaa nyumbani kidogo, baadaye nitakuwa na safari ya mapumziko na familia,” alisema.

Alisema anatarajia kurejea nchini baada ya wiki kadhaa, tayari kuanza maandalizi ya kikosi chake.

Brandts ameingoza Yanga kutwaa ubingwa wa Bara ikiwa ni pamoja na kuwafunga watani wao Yanga katika mechi ya mwisho ya ligi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic