May 19, 2013



Mlezi wa Simba, Rahma Al Kharusi amesema amesikitika kuikosa mechi ya watani, Yanga na Simba iliyopigwa jana kwenye Uwanja wa Taifa.

Rahma maarufu kama Malkia wa nyuki, amesema alipania kuja nchini kuiona mechi hiyo lakini ilishindikana.

“Nilibanwa na majukumu kadhaa yakiwemo mengine ya kiserikali hapa Oman, hivyo nikashindwa kuja.


“Najua Simba wamepoteza mchezo, lakini bado nasisitiza lazima Simba tujipange kwa ajili ya msimu ujao. Tayari wenzetu Yanga walikuwa vizuri, hivyo hatuna jana ya kusikitika sana.

“Tuangalie programu yetu ni nini na kitu gani cha maana ambacho tunafanya,” alisema.

Malkia wa nyuki ndiye amekuwa nguzo ya Simba kwa kushirikiana na kundi la Friends of Simba kuhakikisha klabu hiyo inarudisha heshima yake baada ya kuwa imeyumba chini ya uongozi wa Aden Rage.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic