Short akiwa na Malkia wa nyuki katika ndege yake ya kifahari baada ya kufika uwanjani kuwapokea walipowasili mjini Newcastle jioni ya leo wakitokea London... |
Na
Mwandishi Wetu
MMILIKI wa
klabu ya Sunderland, Ellis Short amewafanyia kufuru ya jeuri ya fedha Mlezi wa
klabu hiyo, Rahma Al Kharusi ‘Malkia wa Nyuki’ kwa kumpa ndege binafsi kama
usafiri.
Pamoja na
kupewa ndege hiyo ambayo mamilionea wa Uingereza huzitumia kwa usafiri binafsi Malkia
wa nyuki atakuwepo uwanjani kesho usiku usiku katika viti maalum vya watu
matajiri wakati Sunderland na Kocha Roberto Di Canio watakapokuwa wanawavaa
Stoke City katika Ligi Kuu England wakipambana kukwepa kuteremka daraja.
Short
ambaye ni mmoja wa mamilionea wa Uingereza, ametoa ndege yake binafsi ya
kifahari na kumkabithi Malkia wa nyuki asafiri nayo kutoka London hadi
Newcastle ambako atakutana naye.
Tayari Short
amefika kwenye uwanja wa ndege Newcastle leo jioni na kumpokea Malkia wa nyuki
ambaye imeelezwa baadaye aliungana na Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage
watakayekuwa pamoja kuanzia leo.
Wakiwa na
ndege hiyo walisafiri kwa zaidi ya kilomita 486 wakiwa angani kabla ya kutua
Newcastle na kukutana na Short.
“Kweli malkia ataondoka leo kutoka London
kwenye Newcastle kwa ajili ya kukutana na mmiliki wa Sunderland ambaye
alimualika kwenda huko.
“Lakini
mwenyekiti Rage naye yuko hapa London na ataondokana naye kwa njia yake hadi
sehemu ambayo watapandia ndege na pale ndiyo ataungana na Malkia wa nyuki, wote
watapanda ndege hiyo ya Short kwenda Newcastle,” kilifafanua chanzo.
“Wakiwa
Newcastle, kwa pamoja watakutana na Short na kufanya naye mazungumzo kuhusiana
na suala la kuanzisha uhusiano lakini pia kuhusiana wa klabu hizo mbili.”
Lakini jioni
hii, Salehjembe, imefanikiwa kumpata Malkia ambaye amesema wamewasili mjini
humo tayari kwa mazungumzo.
“Kila kitu
kinakwenda vizuri, tunatarajia kuwa na mazungumzo ha Short na lengo ni manufaa
ya Simba. Pamoja na hivyo tumealikwa kwa ajili ya mechi ya vijana ambayo Sunderland
watachezaji kesho Jumatatu asubuhi.
“Lakini
usiku kutakuwa na mechi ya Ligi Kuu England watakayocheza dhidi ya Stoke City. Tumealikwa
pia na mazungumzo yetu pia yatafanyika.
“Kwa kuwa
ndiyo nimefika, nafikiri nitazungumza wakati mwingine acha nijiandae na ratiba
ingawa hadi sasa kwa niaba ya Simba namshukuru sana Short kwa kuwa ametupokea
vizuri na tulisafiri na ndege yake kutokea London,” alisema Malkia wa nyuki.
Lengo ni
kuanzisha uhusiano na kusaidiana katika masuala kadhaa yakiwemo ya ushauri wa
kifundi na mengine.
Awali Simba
iliwahi kutumia jina la Sunderland kabla ya kubadilisha mengine kadhaa na kuwa
Simba ambalo linatumika hadi leo.
0 COMMENTS:
Post a Comment