May 13, 2013




Mtanzania Yona Elias Ndabila amezua jambo nchini Nepal baada ya timu yake ya Sarswoti Youth Club kugomea usajili wake.

Pamoja na timu kubwa ya Manange kuamua kutoa dau kubwa ambalo hata hivyo halijawekwa wazi, uongozi wa Sarswoti uligoma.

Mjadala huo ulikuwa mkubwa na kuzua gumzo katika soka nchini humo lakini mwisho Manange imefanikiwa kumnasa Ndabila, mshambuliaji wa zamani wa Prisons na Mtibwa Sugar.


Rais wa Manange, Jamling Ghale amethibitisha kuwa Ndabila ameishamwaga wino katika timu hiyo.

Salehjembe ilikuwa ya kwanza kueleza kuhusiana na Ndabila kujiunga na timu hiyo kabla ya tafrani hilo la usajili.

Ndabila amesema tayari yuko katika kambi ya timu yake mpya na anafanya mazoezi kwa juhudi kujiandaa na michuano ya Gurkha Cup.

Msimu uliopita wa ligi ya Nepal, Ndabila alishika nafasi ya pili kwa kupachika mabao baada ya kufunga 17 lakini alifanikiwa kupachika sita pekee walipokutana na timu ya Bansbari.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic