May 13, 2013




Waliokuwa mabingwa wa Tanzania Bara, Simba wametua mjini Unguja na wapishi wao mjini Unguja kwa ajili ya kambi.

Simba imetua Unguja tayari kujiwinda kwa mechi yao dhidi ya Yanga, Mei 18 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.


Yanga inajiandaa kucheza na Yanga katika mechi ambayo tayari joto lake limepanda kwa kasi ya kimondo.

Uamuzi wa Simba kutua na wapishi wake Unguja inaonekana ni hofu ya kuwa na hujuma.


Lakini Kocha Mkuu, Patrick Liewig akasema huo ni sehemu ya mfumo wa wao kutaka kujitegemea zaidi na wachezaji wao kupata wanachotaka.

“Ni kitu cha kawaida kabisa, hakuna haja ya kuanza kufikiria kuhusiana na hujuma.

“Hata kama ingekuwa hivyo, hakuna ambaye angeweza kupata nafasi ya kutuhujumu na tunajiandaa vizuri kabisa,” alisema Liewig.

Simba iko katika nafasi ya tatu wakati Yanga tayari ni mabingwa na Azam FC iko katika nafasi ya tatu.

Mechi hiyo kwa Yanga ni sehemu ya kutaka kulipa kisasi baada ya kumaliza msimu uliopita kwa kipigo cha mabao 5-0 kutoka kwa Simba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic