May 13, 2013



Nyota wa zamani wa Simba, Emmanuel Okwi bado anaendelea kupambana kupata namba katika kikosi cha kwanza cha timu yake mpya ya Etoile du Sahel ya Tunisia.

Pamoja na benchi la ufundi kuonyesha kumkubali, lakini bado halijamuamini kiasi cha kumpa nafasi 11 za kwanza kikosi kinachopangwa.


Tayari Okwi raia wa Uganda ameshafunga bao moja maridadi katika mechi moja lakini bado linaonekana halijatosha kulishawishi benchi hilo la ufundi.

Lakini Okwi amendelea kufanya mazoezi kwa juhudi na huenda wanaamini atapata nafasi hapo baadaye.

Ushindani wa namba katika kikosi hicho uko juu, ingawa Okwi anaweza kupata nafasi katika kikosi cha kwanza kama ataendelea kupambana.

Aliondoka nchini akiwa tegemeo la Simba na namba katika kikosi cha kwanza haikuwa na maswali hata kidogo.

Simba ambayo pamoja na kumkosa, inaendelea kudai fedha zake dola 300,000 ilizomuuza kiungo huyo mshambuliaji kwa Waarabu wa Tunisia bila ya mafanikio.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic