May 14, 2013


 
Shekhan, kushoto akiwa mazoezini na Kilimanjaro Stars, kulia ni William John aliyewahi kucheza Simba...
Kiungo nyota wa zamani wa Simba, Shekhan Rashid amewaonya Simba kutokana na mwenendo wanaokwenda nao.

Shekhan ambaye anaishi jijini Stockholm, Sweden amesema Simba inaweza kubadilika na kuwa bora lakini kama uongozi utajirekebisha na kuendesha mambo vizuri.

Pamoja na hivyo, kiungo huyo ambaye alikuwa anasifika kwa kupiga pasi ‘rula’ amesema ushirikiano na kupendana baina ya wachezaji kutaifanya Simba irejee katika hali yake.


“Mimi niko mbali huku, lakini ninaamini kama uongozi utafanya kazi yake vizuri, basi mambo yatakwenda vizuri tu na Simba itarudi katika hali yake.

“Lakini suala la umoja, upendo kati ya wachezaji, benchi la ufundi na wote wanaohusika na timu ni kitu muhimu sana,” alisema Shekhan ambaye ni baba wa watoto wawili.

Je, unataka kujua anafanya nini nchini humo, anaendelea na soka au maisha yake yako vipi? Soma baadaye makala inayohusu maisha yake na kila kitu kuhusiana na kiungo huyo nyota wa zamanio wa Wekundu wa Msimbazi ambaye alianzia Yanga ambao walimdharau, akatua Simba na kutisha.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic