May 1, 2013




Yanga waliahidi watakuwa na sapraiz leo kwenye uwanja wa taifa na haijawahi kutokea katika soka la Bongo.

Kumbe walichopanga kufanya ni hiki, hata kabla ya wachezaji kupasha misuri, walizunguka uwanja wakiwapigia makofi mashabiki wao.
Wachezaji pamoja na safu nzima ya benchi la ufundi ilifanya hivyo kuonyesha shukurani kwa mashabiki waliowasapoti hadi kutwaa ubingwa.

Lakini pamoja na kufanya staili hiyo mpya ya ‘kisasa’, Yanga hawakuthubutu hata kidogo kupitiliza upande wa pili wa uwanja ambako kuna rangi nyekundu na nyeupe.


Ilionekana huenda ‘watatia maguu’ kuwashukuru watani wao ambao walikuwa wakihudhuria mechi zao nyingi tu. Lakini wapi, walipokaribia tu upande wa pili, sauti zikaanza kupazwa zikionyesha kwamba wasingependa wafike upande huo.

Yanga nao wakaonyesha wala hawakuwa na mpango wa kuvuka hadi anga za watani, hivyo wakakata kona na kurejea upande wao huku wakishangiliwa na mashabiki wao waliokuwa wamesimama na kuwapigia makofi kujibu walichokuwa wanakifanya.

Yanga imefanikiwa kutwaa ubingwa ikiwa na mechi mbili mkononi, hiyo ya leo dhidi ya Coastal Union na ile la Mei 15 dhidi ya watani wao Simba ambayo inasubiriwa kwa hamu kubwa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic