May 13, 2013




Mazoezi ya Yanga yameendelea kuwa kivutio mjini Pemba kutokana na watu wengi kujitokeza kuyaangalia.

Pamoja na hivyo, mashabiki wengi wanaojitokeza katika Uwanja wa Gombani, wameonyesha kuridhishwa na kiwango wanachokionyesha Yanga.


Mazoezi hayo chini ya Mholanzi, Ernie Brandts yamekuwa yakiwavutia watu wengi na kujenga imani zaidi.

Mashabiki wengi wa Yanga waliopata nafasi ya kuona mazoezi hayo wamekuwa wakijenga imani kwamba lazima Simba italala katika mechi ya Mei 18.


Wengi wanaamini Simba itafungwa kwa kuwa wachezaji wanaonekana wako katika hali nzuri zaidi.

Lakini Yanga wameonyesha asilimia kubwa ya mazoezi yao kuwa siri wakihofia hujuma.

Yanga imeweka kambi mjini hapa na kuzua gumzo huku baadhi ya mashabiki wakionyesha kufurahishwa na uamuzi wa Yanga kuweka kambi Pemba wakati Simba wako Unguja.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic